KAMATI ya maadili imemfungia Afisa Habari wa timu ya Simba Haji
Manara kutojihusisha na shughuli za Mpira ndani na nje ya nchi kwa muda
wa miezi kumi na mbili (12) sawa na mwaka mmoja na faini ya shilingi
milioni tisa (9) kutokana na kukutwa na hatia kwenye makosa yote matatu
aliyokuwa akikabiliwa nayo.
TFF ilimfungulia mashtaka ya kinidhamu yenye makosa matatu kwenye
kamati ya maadili. Kosa la kwanza ni kuongea maneno ya kashfa kwa
viongozi wa TFF, kosa la pili kuchochea ukabila na kosa la tatu ni
kukosoa maamuzi ya TFF kupeleka suala la Mohammed Fakhi kwenye kamati ya
Katiba, Sheria na hadhi za wachezaji.
Mwenyekiti wa Kamati ya nidhamu Jerome Msemwa akitangaza hukumu hiyo
alisema katika shitaka la kwanza Manara amefungiwa mwaka mmoja na faini
milioni moja wakati lile la pili amefungiwa miezi mitatu faini milioni
tatu na la tatu amepigwa faini ya milioni tano au kutojihusisha na soka
kwa miaka saba.
Jerome alisema mshitakiwa alipewa hati ya mashitaka na kutakiwa
kuhudhuria kwenye kikao hicho lakini alishindwa kutokea bila kuwa na
sababu za msingi. Ila Manara yuko huru kukata rufaa kama hajaridhishwa
na hukumu hiyo.
Manara amekutana na kitanzi cha TFF
Title: Manara amekutana na kitanzi cha TFF
Author: Barnicoz Tech
Rating 5 of 5 Des:
Author: Barnicoz Tech
Rating 5 of 5 Des:
KAMATI ya maadili imemfungia Afisa Habari wa timu ya Simba Haji Manara kutojihusisha na shughuli za Mpira ndani na nje ya nchi kwa muda ...
Post a Comment