WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Waziri wa Nishati na Madini, Profesa
Sospeter Muhongo kuhakikisha eneo la Kisarawe II linakuwa na umeme wa
uhakika ili kuwezesha viwanda na wananchi wa eneo hilo kupata nishati
hiyo.
Alitoa
agizo hilo jana jioni (Jumanne, Januari 3, 2017) wakati alipotembelea
kiwanda cha Milkcom kinachozalisha bidhaa za maziwa na kiwanda cha
Watercom kinachozalisha maji vilivyoko katika kata ya Kisarawe ii
wilayani Kigamboni akiwa katika ziara yake ya kikazi.
“Waziri
wa Nishati ahakikishe eneo hili linapata umeme wa uhakika ili
kuviwezesha viwanda hivi kufanyakazi vizuri jambo litakaloongeza
uzalishaji. Pia wananchi wanaoishi katika maeneo haya nao watanufaika na
upatikanaji wa nishati hiyo,” alisema.
Waziri
Mkuu alisema amefarijika na jitihada za muwekezaji huyo za kuungamkono
mkakati wa Serikali ya awamu ya Tano wa kuifanya Tanzania kujenga uchumi
wa viwanda utakaoliwezesha Taifa kufikia uchumi wa kipato cha kati
ifikapo mwaka 2025.
Awali,
Msemaji wa Viwanda hivyo, Aboubakar Faraj akisoma taarifa ya viwanda
hivyo kwa Waziri Mkuu alisema moja ya changamoto zinazowakabili ni
pamoja na upatikanaji wa umeme wa uhakika jambo linasababisha kupanda
kwa gharama za uzalishaji.
“Punde
umeme unapokatika tunalazimika kutumia majenereta kwa muda mrefu. Hii
husababisha ongezeko la gharama za uzalishaji ambazo huumiza kiwanda kwa
sababu haiwezekani kumtwisha mzigo huu mlaji,” alisema.
Faraji
alisema changamoto nyingine ni miundombinu ya barabara ambayo
usababisha wateja wengi kushindwa kufika kwenye viwanda hivyo kwa
urahisi, hivyo aliiomba Serikali kuwatatulia kero hilo.
Aliongeza
kuwa kwa sasa viwanda hivyo vimeajiri watu zaidi ya 1,800, ambapo
alisema endapo Serikali itawahakikishia upatikanaji wa umeme na barabara
wataongeza ajira kwa asilimia 25 ifikapo mwaka 2018.
Mapema Waziri
Mkuu alizindua wodi ya wazazi katika Zahanati ya Kisarawe ii
iliyojengwa kwa ufadhili wa kampuni ya mafuta ya Oilcom. Wodi hiyo yenye
vyumba vitatu itawapunguzia akinamama kusafiri umbali mrefu kutuata
huduma hiyo.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
About Author
The part time Blogger love to blog on various categories like Web Development, SEO Guide, Tips and Tricks, Android Stuff, etc including Linux Hacking Tricks and tips. A Blogger Template Designer; designed many popular themes.
Advertisement

Related Posts
- Zanzibar to Organize a Half Marathon race to Promote Gender Mainstreaming, Attain Sustainable Development Goal06 Jan 20180
More than 300 Zanzibari women, men, girls and boys are expected to participate in t...Read more »
- Embassy of Kuwait in Tanzania Committed to Support Educational Projects in Zanzibar18 Dec 20170
Member of the House of Representative in Zanzibar, Hon Simai Mohammed Said in discussion ...Read more »
- Turkey to intensify relationship with SUZA16 Aug 20170
Delegation of Presidency for Turks Abroad and Related Communities (YTB) meets Prof. Rai (...Read more »
- RAIS DKT. MAGUFULI PAMOJA NA MKEWE MAMA JANETH WATEMBELEA KUWAJULIA HALI WAGONJWA KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI JIJINI DAR ES SALAAM28 May 20170
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamo...Read more »
- Halmashauri kunufaika na Tsh 250 bilioni za mradi wa maji vijijini18 May 20170
Halmashauri za wilaya zimetakiwa kuongeza ufanisi katika kusimamia miradi ya maji kwa kucha...Read more »
- NAIBU MKURUGENZI WA IMF AKUNWA NA UKUAJI WA UCHUMI WA TANZANIA, AAHIDI KUFUNGUA DIRISHA LA MIKOPO KWA TANZANIA18 May 20170
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (wa tatu kulia) akiel...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.