|
Home
»
habarizakitaifa
» TUNISIA YARIDHIA TAMKO KURUHUSU WATU BINAFSI KUPELEKA KESI ZAO MOJA KWA MOJA KWENYE MAHAKAMA YA AFRIKA IILIYO JIJINI ARUSHA Tunisia imesema Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (AfCHPR) ni lazima itangazwe kwa nguvu zote ili kuwawezesha wananchi barani Afrika kufahamu uwepo wake,malengo ya kuanzishwa kwake pamoja na shughuli zake. Akipokea ujumbe wa Mahakama hiyo katika Ikulu ya Tunisia,Rais wa Nchi Hiyo ,Mh.Beji Caid Essebsi alipongeza uanzishwaji wa Mahakama hiyo na kuongeza kuwa inahakikisha ulinzi wa Haki za Binadamu Barani Afrika. “Kwa njia hii,Haki za Binadamu Barani Afrika zitalindwa na kuhakikisha maendeleo endelevu ya demokrasia kwa wananchi” Aliuambia ujumbe huo uliohusisha majaji watatu akiwemo Rais wa AfCHPR,Jaji Sylvain Ore’. Kwa upande wake Rais wa AfCHPR, Jaji Ore’ aliishukuru serikali ya Tunisia kwa kukubali kuupokea ujumbe wake na kukutana na Viongozi na Maafisa mbalimbali wa nchi hiyo na pia kuendesha semina kwa wadau mbalimbali nchini humo kwa lengo la kuitangaza Mahakama. Wakati wa ziara hiyo,Tunisia ilitia saini tamko la kuruhusu watu binafsi na Mashirika yasiyo ya kiserikali(NGO’s) katika nchi hiyo kupeleka kesi zao moja kwa moja katika Mahakama hiyo yenye Makao yake makuu Jijini Arusha. Hatua hiyo ya Tunisia ambayo ni utekelezaji wa kifungu cha 34(6),Inalifanya Taifa hilo kuwa Nchi ya nane Barani Afrika kukubali makundi hayo kupeleka kesi katika Mamlaka za Mahakama hiyo. Nchi nyingine ambazo ni Wanachama wa umoja wa Afrika zilizotoa tamko kukubali Watu binafsi na NGO’s kutoka katika Nchi zao kupeleka kesi katika AfCHPR ni pamoja na:Benin,Burkina Faso,Côte d’Ivoire,Ghana,Malawi,Mali na Tanzania. Utiwaji saini wa tamko hilo ulifanywa na Waziri wa mashauri ya kigeni wa Tunisia,Mh.Khemaies Jhinaoui kwa niaba ya Serikali ya Nchi yake. Rwanda ambayo hapo awali ilitia saini kukubali tamko hilo sasa imejitoa ingawa Mkutano wa Kilele wa Viongozi wa Umoja wa Afrika uliofanyika Addis Ababa,Ethiopia mapema mwaka huu uliitaka nchi hiyo kutafakari juu ya uamuzi wake huo. Kwa upande wake Misri ambayo haijaridhia itifaki iliyoanzisha Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu ilieleza kuridhishwa kwake na utekelezaji wa shughuli za Mahakama hiyo katika kipindi cha miaka 10 iliyopita na kuahidi kuwa itaridhia itifaki husika. Mahakama hiyo ilifanya ziara ya kikazi Nchini Tunisia na Misri kuanzia April 9 hadi 14 Mwaka huu kwa lengo la kukuza uelewa wa wadau mbalimbali juu ya uwepo ya Mahakama,Malengo yake na shughuli zake. Tangu mwaka 2010,AfCHPR imefanikiwa kuendesha ziara 27 za kuelimisha katika Maeneo mbalimbali Barani Afrika na kuendesha Semina na Mikutano ili kukuza uelewa wa Masuala kuhusu ulinzi wa Haki za Binadamu Barani humo na kuhamasisha Nchi wanachama wa AU kuridhia mkataba ulioanzisha Mahakama hiyo na kutoa tamko la kuruhusu watu binafsi na NGO’s kupeleka kesi zao Mahakamani hapo. AfCHPR ilianzishwa na Nchi wanachama wa Umoja wa Afrika(AU) kwa mujibu wa kifungu namba 1 cha itifaki ya Mkataba ya Mahakama hiyo na ilianza shughuli zake rasmi Novemba,2006 kwa lengo la kuimarisha Haki za Binadamu na Watu Barani Afrika.
Tunisia
imesema Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (AfCHPR) ni
lazima itangazwe kwa nguvu zote ili kuwawezesha wananchi barani Afrika
kufahamu uwepo wake,malengo ya kuanzishwa kwake pamoja na shughuli zake.
Akipokea
ujumbe wa Mahakama hiyo katika Ikulu ya Tunisia,Rais wa Nchi Hiyo
,Mh.Beji Caid Essebsi alipongeza uanzishwaji wa Mahakama hiyo na
kuongeza kuwa inahakikisha ulinzi wa Haki za Binadamu Barani
Afrika.
“Kwa
njia hii,Haki za Binadamu Barani Afrika zitalindwa na kuhakikisha
maendeleo endelevu ya demokrasia kwa wananchi” Aliuambia ujumbe huo
uliohusisha majaji watatu akiwemo Rais wa AfCHPR,Jaji Sylvain Ore’.
Kwa
upande wake Rais wa AfCHPR, Jaji Ore’ aliishukuru serikali ya Tunisia
kwa kukubali kuupokea ujumbe wake na kukutana na Viongozi na Maafisa
mbalimbali wa nchi hiyo na pia kuendesha semina kwa wadau mbalimbali
nchini humo kwa lengo la kuitangaza Mahakama.
Wakati
wa ziara hiyo,Tunisia ilitia saini tamko la kuruhusu watu binafsi na
Mashirika yasiyo ya kiserikali(NGO’s) katika nchi hiyo kupeleka kesi zao
moja kwa moja katika Mahakama hiyo yenye Makao yake makuu Jijini
Arusha.
Hatua
hiyo ya Tunisia ambayo ni utekelezaji wa kifungu cha 34(6),Inalifanya
Taifa hilo kuwa Nchi ya nane Barani Afrika kukubali makundi hayo
kupeleka kesi katika Mamlaka za Mahakama hiyo.
Nchi
nyingine ambazo ni Wanachama wa umoja wa Afrika zilizotoa tamko
kukubali Watu binafsi na NGO’s kutoka katika Nchi zao kupeleka kesi
katika AfCHPR ni pamoja na:Benin,Burkina Faso,Côte
d’Ivoire,Ghana,Malawi,Mali na Tanzania.
Utiwaji
saini wa tamko hilo ulifanywa na Waziri wa mashauri ya kigeni wa
Tunisia,Mh.Khemaies Jhinaoui kwa niaba ya Serikali ya Nchi yake.
Rwanda
ambayo hapo awali ilitia saini kukubali tamko hilo sasa imejitoa ingawa
Mkutano wa Kilele wa Viongozi wa Umoja wa Afrika uliofanyika Addis
Ababa,Ethiopia mapema mwaka huu uliitaka nchi hiyo kutafakari juu ya
uamuzi wake huo.
Kwa
upande wake Misri ambayo haijaridhia itifaki iliyoanzisha Mahakama ya
Afrika ya Haki za Binadamu na Watu ilieleza kuridhishwa kwake na
utekelezaji wa shughuli za Mahakama hiyo katika kipindi cha miaka 10
iliyopita na kuahidi kuwa itaridhia itifaki husika.
Mahakama
hiyo ilifanya ziara ya kikazi Nchini Tunisia na Misri kuanzia April 9
hadi 14 Mwaka huu kwa lengo la kukuza uelewa wa wadau mbalimbali juu ya
uwepo ya Mahakama,Malengo yake na shughuli zake.
Tangu
mwaka 2010,AfCHPR imefanikiwa kuendesha ziara 27 za kuelimisha katika
Maeneo mbalimbali Barani Afrika na kuendesha Semina na Mikutano ili
kukuza uelewa wa Masuala kuhusu ulinzi wa Haki za Binadamu Barani humo
na kuhamasisha Nchi wanachama wa AU kuridhia mkataba ulioanzisha
Mahakama hiyo na kutoa tamko la kuruhusu watu binafsi na NGO’s kupeleka
kesi zao Mahakamani hapo.
AfCHPR
ilianzishwa na Nchi wanachama wa Umoja wa Afrika(AU) kwa mujibu wa
kifungu namba 1 cha itifaki ya Mkataba ya Mahakama hiyo na ilianza
shughuli zake rasmi Novemba,2006 kwa lengo la kuimarisha Haki za
Binadamu na Watu Barani Afrika.
About Author
The part time Blogger love to blog on various categories like Web Development, SEO Guide, Tips and Tricks, Android Stuff, etc including Linux Hacking Tricks and tips. A Blogger Template Designer; designed many popular themes.
Advertisement

Related Posts
- Zanzibar to Organize a Half Marathon race to Promote Gender Mainstreaming, Attain Sustainable Development Goal06 Jan 20180
More than 300 Zanzibari women, men, girls and boys are expected to participate in t...Read more »
- Embassy of Kuwait in Tanzania Committed to Support Educational Projects in Zanzibar18 Dec 20170
Member of the House of Representative in Zanzibar, Hon Simai Mohammed Said in discussion ...Read more »
- Turkey to intensify relationship with SUZA16 Aug 20170
Delegation of Presidency for Turks Abroad and Related Communities (YTB) meets Prof. Rai (...Read more »
- RAIS DKT. MAGUFULI PAMOJA NA MKEWE MAMA JANETH WATEMBELEA KUWAJULIA HALI WAGONJWA KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI JIJINI DAR ES SALAAM28 May 20170
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamo...Read more »
- Halmashauri kunufaika na Tsh 250 bilioni za mradi wa maji vijijini18 May 20170
Halmashauri za wilaya zimetakiwa kuongeza ufanisi katika kusimamia miradi ya maji kwa kucha...Read more »
- NAIBU MKURUGENZI WA IMF AKUNWA NA UKUAJI WA UCHUMI WA TANZANIA, AAHIDI KUFUNGUA DIRISHA LA MIKOPO KWA TANZANIA18 May 20170
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (wa tatu kulia) akiel...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.