Barnicoz Tech Barnicoz Tech Author
Title: Mwanariadha Alphonce Simbu atoa siri ya Ushindi baada ya Kutua Nchini.
Author: Barnicoz Tech
Rating 5 of 5 Des:
Baada ya kutua nchini jana akitokea nchini Uingereza kutoka kwenye Mashindano ya Riadha ya London Marathon, mwanariadha Mtanzania Alphonce ...
Baada ya kutua nchini jana akitokea nchini Uingereza kutoka kwenye Mashindano ya Riadha ya London Marathon, mwanariadha Mtanzania Alphonce Felix Simbu ameeleza kuwa siri ya mafanikio yake ya kufanya vizuri katika mashindano hayo yaliyomalizika hivi karibuni nchini Uingereza, ni Juhudi na kujituma zaidi katika mazoezi.

Simbu, ambaye alishika nafasi ya 5 katika mashindano hayo makubwa Duniani, amewataka wakimbiza upepo wengine wenye ndoto kama zake ni lazima wafanye mazoezi kwa juhudi kabla ya kushiriki mashindano yoyote makubwa. Ameyasema hayo katika hafla fupi ya kumpongeza huko Mkoani Arusha.
Hata hivyo nyota huyo anayeiwakilisha vyema taifa, katika mchezo wa riadha siku za hivi karibuni amewataka wadau wajitokeze kushirikiana na serikali kuwekeza zaidi katika mchezo huo, kwani yeye ni jibu tosha la zao lililopatikana katika uwekezaji wa muda mfupi.
Felix Simbu ametumia saa 2, dakika 9 na sekunde 9 na kushika nafasi hiyo ya tano.
Ambapo inaonyesha mwanariadha anayeshika nafasi ya tano katika mashindano hayo anaibuka na kitita cha dola 10,000 (zaidi ya Sh milioni 22).

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top