Barnicoz Tech Barnicoz Tech Author
Title: Messi airudisha Barcelona kwenye mbio za Ubingwa wa La Liga
Author: Barnicoz Tech
Rating 5 of 5 Des:
Usiku wa jana April 23 kulikuwa na mchezo wa El Classico, mchezo ambao ulitabiriwa kuamua bingwa wa ligi hiyo (La Liga) kutokana na endap...

Usiku wa jana April 23 kulikuwa na mchezo wa El Classico, mchezo ambao ulitabiriwa kuamua bingwa wa ligi hiyo (La Liga) kutokana na endapo Real Madrid ingeshinda mchezo huo ingeweza kumshinda mpinzani wake kwa tofauti ya point 6 pamoja na mchezo mmoja mkonini, kitu ambacho ingekuwa ni vigumu kwa Barcelona kumpindua mpinzani wake huyo kileleni kutokana na michezo ambayo imebaki katika ligi hiyo.
Chachu kubwa ya ushindi wa Barcelona katika mchezo wa jana ni mshambuliaji wake machachari Leonel Messi ambaye alicheza mpira mwingi sana katika mchezo huo na kufanikiwa kuipachikia timu yake mabao mawili kati ya 3 ambayo timu hiyo ili yapata dhidi ya 2 ya Real Madrid.
Ushindi huo umeiwezesha Barcelona kukaa kileleni kwa muda huku yakisubuirwa matokeo ya mchezo mmoja wa mkononi wa Real Madrid.
Msimamo wa La Liga
Lolote linaweza kutokea katika ligi hiyo kwasasa, niandikie maoni yako, ni nani unahisi atakuwa bingwa wa ligi hiyo msimu huu? Uwanja wa comments unakuhusu.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top