Barnicoz Tech Barnicoz Tech Author
Title: Serengeti Boys imepata ushindi dhidi ya wenyeji wa AFCON U-17
Author: Barnicoz Tech
Rating 5 of 5 Des:
Timu ya taifa ya Tanzania ya vijana chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ imepata ushindi wa magoli 2-1 kwenye mchezo w kirafiki wa kujipim...
Timu ya taifa ya Tanzania ya vijana chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ imepata ushindi wa magoli 2-1 kwenye mchezo w kirafiki wa kujipima nguvu dhidi ya Gabon ambao ni wenyeji wa michuano ya AFCON U-17 2017.
Mechi hiyo imepigwa nchini Morocco ambapo Serengeti Boys imeweka kambi kwa ajili ya maandalizi ya michuano vijana wa chini ya miaka 17 iyopangwa kufanyika Gabon kuanzia Mei 14 mwaka huu.
Magoli ya Serengeti Boys yamefungwa na Kelvin Nashoni na Ibrahim Abdallah Ally.
Shaffihdauda.co.tz inaungana na watanzania wote kuitakia kila la heri Serengeti Boys iendelee kujiandaa vyema ili iwakilishe taifa vizuri katika michuano hiyo ya vijana.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top