
Magufuli ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza mara baada ya
kuwaapisha viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi,
Jenerali Vanance Mabeyo pamoja na viongozi wengine wa majeshi, na
mabalozi.
Katika hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu jijini Dar es
Salaam, Rais Magufuli alianza kwa kumpongeza Mkuu wa Jeshi la Polisi
Nchini (IGP), Ernest Mangu kwa hatua nzuri aliyoichukuwa ya
kuwasimamisha kazi Askari Polisi 12 waliotuhumiwa kujihusisha na dawa za
kulevya ili kupisha uchunguzi.
Rais Magufulia amesema hakuna wa kuachwa hata akiwa mkewe Mama Janet
Magufuli, na kuongeza kuwa wakamatwe bila ya kujali majina yao.
"Najua IGP Mangu watu walikupigia simu wanakupa ushauri kuhusu Dawa za Kulevya, ungewasikiliza leo usingekuwa IGP.
"Vita ya dawa za kulevya haina cha umaarufu, haijalishi ni mtoto wa nani anahusika, hata kama ni mke wangu mkamateni.
"IGP nakuagiza kamata watuamiaji wote wa dawa za kulevya hao watakwambia
wanapozipata, haiwezekani ziuzwe kama njugu",amesema Rais Magufuli
Akizungumzia suala la uendeshaji wa kesi za dawa kulevya, Rais Dkt
Magufuli amemwambia Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania, Jaji Prof. Ibrahim
Hamis Juma kuwa kesi hizo zinaendehswa taratibu sana huku akitolea mfano
wa mfanyabiashara mmoja maarufu wa dawa za kulevya aliyekamatwa mkoani
Lindi lakini hakuwahi kufikishwa mahakamani.
"Kuna mfanyabiashara maarufu wa dawa za kulevya alikamatwa mkoani Lindi
lakini sijawahi kusikia amefikishwa mahakamani" Amesema Rais Magufuli.
Rais Magufuli amesema kuwa vita ya dawa za kulevya si ya Paul Makonda
peke yake bali ni ya Watanzania wote huku akivitaka vyombo mbalimbali
vya ulinzi na usalama kushirikiana kutokomeza tatizo hili linalopelekea
kupoteza nguvu kubwa ya taifa.
Kauli hii ya Rais Magufuli inakuja ikiwa ni siku chache tangu Mkuu wa
Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda atangaze vita dhidi ya watu
wanaohusika na dawa za kulevya akianza kwa kutaja majina yakiwemo ya
askari na ya wasanii maarufu wa muziki na filamu akiwemo Wema Sepetu,
Chid Benz, Vanessa Mde n.k.
Siku tatu baada ya Makonda kuwataja watuhumiwa hao, IGP Ernest Mangu
alichukua hatua ya kuwasimamisha askari 12 waliotajwa na kuahidi
kuchukua hatua zaidi, jambo ambalo limepongezwa na Rais Magufuli na
kumueleza kuwa endapo asingechukua hatua hiyo, angejua kuwa na yeye
anahusika.
Post a Comment